Friday, July 7, 2017

Kortini akidaiwa kulawiti wanafunzi


HALID Mohamed (28) amefi kishwa Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Igunga kwa tuhuma ya kulawiti wanafunzi wawili wa shule ya msingi Chipukizi wilayani hapa.

Mwendesha Mashitaka wa Polisi Wilaya ya Igunga, Elimajid Kweyamba aliiambia mahakama mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Ajali Milanzi kuwa shitaka la kwanza linalomkabili mshitakiwa huyo lilitokea kati ya Februari 1 mpaka 14 mwaka huu.

Alisema katika Mtaa wa Uarabuni mjini Igunga mshitakiwa alimlawiti mwanafunzi mwenye miaka 9 wa kiume anayesoma darasa la pili shule ya msingi Chipukizi na kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri.

Aliongeza kwamba shitaka la pili lilitendeka kati ya Februari 1 hadi 14 vilevile katika mtaa huohuo ambapo mshitakiwa alimlawiti mwanafunzi wa miaka 7 wa kiume anayesoma darasa la pili katika shule hiyo hiyo ya Chipukizi.

No comments:

Post a Comment